Skip to main content

SHAIRI-UTU UMEJAA KUTU

UTU UMEJAA KUTU



Ziko wapi zama za kale,nilizozisikia kule Nambale
Undugu ulikuwa kufaana,haukuwa katu kufanana
Ukarimu kwa kila mja,kusaidiana nambari moja
Mambo keshageuka,utu umejaa kutu.

Fukara wateseka,wenye navyo wana makeke
Maradhi keshavamia,wachochole hawana nia
Wamekuwa tangatanga,ombaomba  jina lao
Mambo keshageuka, utu umejaa kutu

Mabwenyenye wajionyesha,wasaidiapo walalahoi
Pale mitandaoni,picha zatamba anuwai
Wanazopiga na kuposti,wakipeana yao misaada
Mambo keshageuka, utu umejaa kutu.
Spencerpenfam©2020

malenga mpole
SHARON OBANDA
SPPF

Comments

Popular posts from this blog

SHAIRI-KIRUSI GIZA

KIRUSI GIZANI

WAMJUA FRANCIS?

Francis Wakhu Omusula alizaliwa mnamo tarehe 18 mwezi wa januari mwaka wa 1996 katika kaunti ya Kakamega (037); kaunti ndogo ya Butere ; Kanda ya Buchenya. Yeye ni mzaliwa wa nne kwa familia ya watoto Saba. Francis alianza masomo yake ya chekechea mnamo mwaka wa elfu mbili na mbili  katika shule ya msingi ya Bululwe ambapo aliufanya mtihani wake wa kitaifa wa darasa la nane huko na kuweza kunyofoa alama bora. Baada ya hapo, alijiunga na shule ya upili ya Shibanga kule Butere na kuwa mojawapo wa waanzilishi waliofuzu vyema kutoka ile shule. Baada ya hapo, Francis alikuwa na ari ya tamaa ya kuwa mwalimu. Alijiunga na Chuo kikuu Cha Mount Kenya mwaka wa 2016 septemba na kufuzu na First Class Honours katika shahada ya ualimu( Kiswahili na Historia). Pia , aliweza kupata tuzo la  mwanafunzi bora wa kiume kati ya maghafali waliofuzu katika hicho chuo Cha MKU (Kitengo Cha  Fadhili la serikali) Francis aliwahifunza Shule ya akademia ya Butere Pace Junior, Shule ya up...