Skip to main content

SHAIRI-KIRUSI GIZA

KIRUSI GIZANI



Hii ni yangu barua,japo isiyo rasmi
Kubali kuipokea, uinusuru jamii
Magoti naangukia,Mola jibu langu ombi
Limetuingia Giza, kirusi korona giza

Naita tena naita, milimani kiangalia
Ewe Mungu nakwita,sikia na angalia
Duniani Kuna nta, ya uwele usosikia
Limetuingia giza,kirusi korona giza

Labda ni mwisho,wa sayari  ya tatu
Dunia ina vitisho,vimejaa matu
Uwele hauna bisho,hii sayari ya watu
Limetuingia giza, kirusi korona giza

Yameshinda na uchina,wanalia Italia
Dunia haina zana,uhai kupigania
Ila tunakazana na,janga hili la Dunia
Limetuingia giza, kirusi korona giza.

Najua tuna ujuzi, wa miili kutibu
Japo uwele u wa juzi, umeshinda matabibu
Kirusi hiki kijuzi, Labda kwako tutubu
Limetuingia giza, kirusi korona giza
Spencerpenfam©2020
#sanitize

EUGENE JOSEPH
SPPF

Comments

Post a Comment

Popular posts from this blog

WAMJUA FRANCIS?

Francis Wakhu Omusula alizaliwa mnamo tarehe 18 mwezi wa januari mwaka wa 1996 katika kaunti ya Kakamega (037); kaunti ndogo ya Butere ; Kanda ya Buchenya. Yeye ni mzaliwa wa nne kwa familia ya watoto Saba. Francis alianza masomo yake ya chekechea mnamo mwaka wa elfu mbili na mbili  katika shule ya msingi ya Bululwe ambapo aliufanya mtihani wake wa kitaifa wa darasa la nane huko na kuweza kunyofoa alama bora. Baada ya hapo, alijiunga na shule ya upili ya Shibanga kule Butere na kuwa mojawapo wa waanzilishi waliofuzu vyema kutoka ile shule. Baada ya hapo, Francis alikuwa na ari ya tamaa ya kuwa mwalimu. Alijiunga na Chuo kikuu Cha Mount Kenya mwaka wa 2016 septemba na kufuzu na First Class Honours katika shahada ya ualimu( Kiswahili na Historia). Pia , aliweza kupata tuzo la  mwanafunzi bora wa kiume kati ya maghafali waliofuzu katika hicho chuo Cha MKU (Kitengo Cha  Fadhili la serikali) Francis aliwahifunza Shule ya akademia ya Butere Pace Junior, Shule ya up...

SHAIRI-UTU UMEJAA KUTU

UTU UMEJAA KUTU